DALILI 7 Za Kuonyesha Anakucheat Na Mwingine..!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


DALILI 7 Za Kuonyesha Anakucheat Na Mwingine..!!

Katika mahusiano huwa kuna changamoto tofauti tofauti. Kwa kawaida ni muhali kupata mahusiano ambayo hayana patashuka moja au nyingine. Inajulikana ya kuwa mahusiano huwa kuna migogoro, kutoelewana, kunyamaziana na mbaya zaidi...vita.

Anyway mambo kama haya huwezi kuyazuia kwa sababu wenyewe ndio wanayaita mapenzi. Utaskia mtu akilalamika kuwa amemiss kugombana ama kuteteshana na mpenzi wake, jambo ambalo huwa ni la kawaida.

Ok. tukija katika mada yetu ni kuwa nataka nikuulize maswali yafuatayo. Je hivi karibuni umeona kama mpenzi wako amekuwa mtu tofauti na ilivyo kawaida? Je mpenzi wako imekuwa muda mrefu tangu mfanye mambo yenu ya kawaida ambayo mlikuwa mkifanya? Je unamshuku kama amepata mwingine?

Kama majibu yako ni NDIO basi hili chapisho nimeliandika spesheli kwako na nataka umakinike kwa kusoma dalili zetu tulizoziandika na kama yote yanawiana na dhana yako basi ni wakati wa kumfungukia mpenzi wako na umwambie kweupe kuwa umechoshwa na tabia yake ya 'kutoka nje', na umuulize kama amechoshwa nawe ili ukate minyororo ya kuwa naye ili uwe huru.

Zama nami!

Dalili #7: Muda mwingi anajaribu kujirembua kuoneka vizuri

Kuvalia vizuri kila wakati si jambo baya la kufanya katika mahusiano, mwanzo wapenzi hupenda sana kuhakikisha ya kuwa wanampendeza mwenza wao.

Lakini, ukiona ya kuwa anamakinika zaidi na upande wa kujifanya aonekane mrembo, basi itakuwa anajaribu kumridhisha mtu mwingine kando na wewe. Kama umemgundua kuwa anajaribu kuvalia vizuri wakati anatembelea hizi sehemu basi weka ? katika mawazo yako: Kazini, supermarket, mkahawa, na hata gym!

Makinika: Zile sehemu zake za kawaida anazozienda kama amezijeuza kuwa fashion show itakuwa ni ishara ya kuwa anakucheat.

Dalili #6: Anakuwa msiri na simu yake, pakatalishi yake nk

Kila mtu ana haki ya kuwa na faragha yake. Mwanzo, watu wengi hawapendi faragha yao ishambuliwe na hata wapendwa wao. But ishu itakuja wakati ambapo anakuwa msiri kuhusu vitu vyake zaidi kuliko awali.

Hii inaweza kumaanisha kuwa kunakuwa na migogoro isioisha wakati ambapo umechukua kuangalia simu yake hadi ule wakati anaudhika wakati umeingia kwa chumba chake akiwa anatumia kompyuta yake. Ukiona mtu akianza kuwa msiri zaidi ni kuwa atakuwa anawasiliana na mchumba mwingine ambaye ako naye.

Dalili #5: Anapunguza hamu ya kufanya tendo la ndoa hadi kukataa asilani

Hata watu waseme nini, kufanya mapenzi ni sehemu muhimu inayohitajika katika mahusiano. Kama hamfanyi mapenzi, utajihisi ya kuwa unabezwa na kukatalika na mpenzi wako.

Wakati umri unaposongea, utagundua ya kuwa kiasi cha mapenzi mnachofanya huwa kinapungua. Hio ni kawaida, lakini kuna hatua nyingine neno 'ni kawaida' linaondolewa.

Kukataliwa katakata kufanya mapenzi ama kutoa visababu inaweza kumaanisha kwa njia rahisi kuwa hajiskii kufanya mapenzi na wewe. Wakati mtu anakucheat, huwa anapoteza ule muungano wa kihisia na wewe na atakuwa hana hamu ya kufanya mapenzi na wewe

Dalili 4: Kuna yule mtu kilinge (mysterious)

Wale watu kilinge ndio unaopaswa kuwaogopa zaidi. Wanaume na wanawake kwa kawaida watakuwa na marafiki wa jinsia ile nyingine, lakini kama utamwona mpenzi wako haachi kuongea kuhusu huyo mtu basi kuna tatizo.

Hata kama nia yake ni nzuri, anaweza kuwa na kitu ambacho ni zaidi ya kuwa marafiki. Kama hatakuruhusu ukutane na huyu mtu kilinge ambaye amekuwa akipoteza muda wake mwingi naye, basi kunaweza kuwa na kitu ambacho ni zaidi ya kuchat pekee.

Dalili #3: Anazozana na wewe zaidi ya kawaida

Kukefyakefya na kukufananisha na wengine ni jambo lisilokubalika katika usuhiano. Wakati ambapo hii itatoka kuanzia mzaha hadi kuwa serious, ni ishara ya kuwa anakucheat.

Mara nyingi, mpenzi akikosana na mwenziwe hujaribu kujitenga na majibizano. Lakini ukiona ya kuwa kila wakati anagombana na wewe kwa sababu ya mahusiano yenu basi ni ishara ya kuwa kuna mwingine ambaye anamwonyesha mapenzi ya dhati...na si wewe

Dalili #2: Anakutenga wewe na marafiki zako wa karibu

Wapenzi wawili ambao wamekuwa pamoja kwa muda mrefu huwa wanagawa marafiki pamoja. Hawa ni wale ambao nyinyi wawili mnawaingiza katika maisha yenu kadri miaka inavyosonga. Wakati umeona kuwa mpenzi wako anapunguza muda wa kuwa na wewe na anachofanya ni kuwatenga watu hawa, kawaida huwa kuna mtu anahusika.

Anaweza kuwa hana moyo wa kukabiliana na marafiki wa karibu na kuwadanganya kuhusu furaha anayopata katika mahusiano yenu. Hii inaweza kutokea baada ya muda mrefu ama akajitenga ghafla.

Dalili #1: Analijeuza neno ''tu'' hadi ''ni'' polepole

Neno ''tu'' katika mahusiano ni takatifu. Huu ni ule wakati ambao mwanaume na mwanamke wamewekeza shina la kuwa pamoja. Wakati mwingi, sana sana wanawake ndio huwa wa kwanza wa kubadilisha neno ''ni'' hadi ''tu'' halafu mwanaume akalizoea.

Hivyo katika mahusiano ukiona mpenzi wako ameanza kurudia kutumia neno ''ni'' itakuwa anajaribu kukutenga katika maisha yake, anajaribu kukufuta katika picha yake.


Mwisho ni kuwa kudanganya katika mahusiano ni swala zito ambalo linaibua hisia nzito, lakini dalili za kucheat zinaweza kutatiza zaidi.

Kukataa kufanya mapenzi ama kujaribu kujirembua inaweza kusababishwa na misongo ama kutojiskia shangwe yeye mwenyewe. Kabla ya kumlaumu kuwa anafanya mabaya, hakikisha ya kuwa kuna ishu inayoendelea, ama inaweza kuwa wewe ndiwe chanzo cha kufanya mahusiano yenu yavunjike
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad