Fahamu mchakato wa kuwapitisha wagombea kwenye kikao cha kamati kuu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Ikiwa imesalia wiki moja kabla ya kampeni za uchaguzi kuanza nchini Tanzania, wawania ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatarajiwa kujua hatma yao hii leo. Chama hicho tawala kiko katika matayarisho ya kuwapata wagombea wake katika ngazi zote baada ya kupitisha wagombea wa urais mwezi uliopita.



Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa nchi, Dkt. John Pombe Magufuli hapo jana aliongoza Kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho, Dodoma, kwa lengo la kuandaa agenda ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa hii leo.

Kikao hicho na cha leo ni mwendelezo wa safari ya CCM kupata wagombea wa nafasi mbali mbali kuelekea uchaguzi wa hapo Oktoba 28.

Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kitakuja na matokeo yasiyotarajiwa kwa baadhi. Yapo majina ambayo yalipita yakiwa ya kwanza kwa kura za wajumbe lakini yatakatwa, badala yake yatapitishwa majina mengine.

Pia, zitashuhudiwa sura mpya kuiwakilisha CCM katika majimbo, huku baadhi ya sura kongwe zikidondoshwa.

Tafsiri ya hilo ni kwamba zile kura za wajumbe sio maamuzi ya mwisho kwa CCM, bali kura hizo hutoa mwongozo wa awali katika kufanikisha mchakato mzima hadi kulipata jina moja la mgombea atakayepambana na wagombea wa vyama vya upinzani.

Kwanini majina hukatwa?

Moja kati ya sababu ya majina kukatwa, hata yale yaliyopata ushindi wa kwanza katika kura za wajumbe ni ushawishi wa mgombea. Vyama vya kisiasa daima hutafuta urahisi wa kushinda. Mgombea ambaye huonekana ni mzigo kwa chama hata kama wajumbe walimpitisha kwa kura nyingi, uwezekano wa kupitishwa katika vikao vinavyofuata unakuwa mgumu sana.

Wanachama wa CCM
Maadili ya mgombea ni jambo jingine linalozingatiwa. Ni karata muhimu kwa wanaosaka nafasi ya kuiwakilisha CCM. Maadili yanaweza kumuinua aliyepata ushindi wa tatu ama wa pili na kumzamisha aliyepata wa kwanza.

Katika mchakato wa uchaguzi wa awali, mambo yalikuwa ya uwazi sana. Kura zilihesabiwa bila kificho, kila mchukua fomu akavuna alichopanda. Licha ya uwazi katika mchakato huo, bado malalamiko kuhusu vitendo vya rushwa yalizuka.Rushwa inaweza kuwa sababu nyingine ya jina la mgombea kukatwa. Wale wanaoshinda kura za wajumbe kwa kutumia mbinu hiyo, ikibainika ni rahisi majina yao kutupwa na kuangaliwa majina mengine yaliyo safi.

Ina maana kuwa, hadi CCM inamkabidhi mgombea wake wa mwisho kuipeperusha bendera ya chama, mchakato na mchujo wa majina unakuwa mrefu sana. Na hiyo ndio siasa ya uchaguzi ndani ya CCM.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad