Mdogo wake Trump afariki dunia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Ndugu yake rais wa Marekani Donald Trump, Robert Trump, amepoteza maisha  hospitalini alipokuwa akipatiwa matibabu mjini New York.

Rais wa Marekani, Donald Trump, ambaye ametoa taarifa ya maandishi juu ya kifo cha kaka yake Robert Trump (72), amesema


"Kwa huzuni kubwa, kaka yangu mpendwa Robert amefariki kwa amani usiku wa kuamkia leo. Alikuwa sio kaka yangu tu, bali pia rafiki yangu mkubwa. Tutakukumbuka sana, lakini siku moja tutakutana tena."


Imeripotiwa kwamba Robert Trump, anayejulikana kwa msaada wake kwa Trump, alikuwa akitibiwa ugonjwa ambao haujafafanuliwa wazi.


Trump alimtembelea kaka yake jana, ambaye alipelekwa hivi karibuni katika Hospitali ya New York-Presbyterian huko Manhattan.


Hakuna taarifa yoyote ambayo imetolewa kutoka kwa mamlaka kuhusu sababu halisi ya kifo cha Robert Trump.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad