CAF Yampongeza CEO Mpya wa Simba...Wanaompinga Mlie tu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



RAIS wa Shirikisho la Soka Afrika, Ahmad Ahmad amemwandikia barua kumpongeza Mtendaji Mkuu (CEO) mpya wa simba, Barbara Gonzalez kwa uteuzi wake akimtakia kila la kheri katika majukumu hayo mapya.

Barbara Gonzalez ni CEO wa kwanza mwanamke kuteuliwa katika klabu za Ligi Kuu Tanzania jambo ambalo limemgusa Rais huyo wa CAF.

Barbara anachukua mikoba ya aliyekuwa CEO wa timu ya Simba, Senzo Mbata ambaye alijiuzulu hivi karibuni na muda mfupi tu picha zilisambaa akiwa na viongozi wa Yanga ambao kwa sasa wamempa dili akiwa ni mshauri mkuu wa klabu hiyo yenye maskani yake pale Jangwani.

Kupitia barua ya pongezi Rais amendika kuwa ni furaha kwake kuona nafasi kubwa ya uongozi kwenye masuala ya michezo akipewa mwanamke jambo linaloweka usawa katika kazi na usawa kwa jinsia.

Pia ameongeza kuwa anakubali uwezo wa CEO mpya na kumtakia kila la kheri katika utendaji wake wa kazi.

Pia CEO huyo alipewa pongezi na Ubalozi wa Marekani wa Tanzania huku ukieleza kuwa umekuwa ukiunga kwa muda mrefu masuala ya wanawake katika uongozi na ndani ya uwanja.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad