Afisa wa polisi aliyemuua mtu mweusi afutwa kazi Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



 

Shaun Lucas, ambaye ni afisa wa polisi aliyehusika na muaji ya mchezaji wa zamani wa American Football Jonathan Price kutumia silaha ya umeme katika jimbo la Texas, ameripotiwa kuachishwa kazi.

Katika maelezo yaliyotolewa na utawala wa Wolfe City, iliarifiwa kuwa afisa huyo katili Lucas mwenye umri wa miaka 22 alifutwa kazi kutokana na mauji hayo.

Maelezo zaidi yanaarifu kuwa utawala wa mji ulimchukulia Lucas hatua hiyo kwa kuzingatia kosa la ‘‘ukiukaji mkubwa’’ wa kanuni za idara ya polisi.

Wakili wa Price, Lee Merritt, alifahamisha kuwa familia yake iliridhishwa na taarifa hizo za kufutwa kazi kwa Lucas, ingawa walitarajia uamuzi huo kuchukuliwa tangu mwanzoni.

Usiku wa Jumamosi baada ya polisi kupewa taarifa za kuzukwa kwa ugomvi nje ya duka moja la ununuzi, Lucas alielekea kwenye eneo la tukio na kutaka kumkamata Price ambaye ni Mmarekani mwenye asili ya Kiafrika.

Price mwenye umri wa miaka 31 alinyanyua mikono hewani na kutaka kujisogeza mbali na polisi. Lucas akamkabili kwa kutumia silaha ya umeme na baadaye akamuua kwa kumpiga risasi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad