Bomu Lililobakia Vita vya pili vya Dunia Lalipuliwa Ujerumani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Bomu lililobaki tangu vita vya pili vya dunia limetangaza kulipuliwa na kuharibiwa katika mji wa Cologne nchini Ujerumani.


Manispaa ya mji wa Cologne ilitoa maelezo na kuarifu kupatikana kwa bomu hilo lenye uzito wa kilo 500 katika kitongoji cha Ehrenfeld, ambalo lililipuliwa na kuharibiwa baada ya wakaazi 13,000 ambao wengi ni Waturuki kuhamishwa kwa muda.


Wakaazi waliohamishwa walipelekwa kwenye uwanja wa mpira wa RheinEnergie wa timu ya mji huo ya FC Cologne.


Bomu hilo liliweza kuharibiwa baada ya tahadhari za usalama kuchukuliwa katika eneo.


Mabomu mengine ambayo yalibakia wakati wa vita vya pili vya dunia yanapatikana katika mitaa mingi ya Ujerumani. Mabomu hayo yamekuwa yakilipuliwa na kuharibiwa na wataalamu kwa tahadhari.


 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad