Joh Makini amuweka kando mdogo wake Nikki wa Pili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii wa HipHop Joh Makini amewataja wasanii kama Lord Eyes, G Nako Warawara na Fid Q kama ndiyo wasanii pekee ambao wapo katika kizazi chake cha marapa wakali Bongo huku akimtoa mdogo wake Nikki wa Pili kwa kusema ana era yake tofauti.


Joh Makini amesema hayo kwenye kipindi cha SalamaNa ya East Africa TV ambayo inaruka kila siku ya Alhamisi kuanzia 3:00 usiku ambapo alikuwa anawataja wasanii wa HipHop ambao anawakubali.


 "Kwenye kizazi changu mimi kuna marapa wakali wengi tu kama Lord Eyes, Gnako na FidQ lakini Nikki wa Pili simuweki hapa, yeye ana 'era' yake pia" amesema Joh Makini 

"Mimi na Lord Eyes tumetoka mbali tangu mihangaiko ya Arusha hadi kuja Dar na kukaa pamoja, hali yake ambayo aliipitia wote ilituhuzunisha lakini na hatukuwa na chakufanya  ulikuwa wakati mgumu kwetu" ameongeza 


Joh Makini, Lord Eyes, Nikki wa Pili na G Nako ni wasanii wa HipHop ambao kwa pamoja wanatokea kwenye kampuni ya Weusi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad