Marekani yaionya China dhidi ya kuivamia Taiwan

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mshauri wa usalama wa taifa nchini Marekani, Robert O'Brien, ameionya China dhidi ya jaribio lolote la kuitwaa Taiwan kwa nguvu, akisema operesheni za kijeshi ya ardhini, baharini na angani huwa ngumu na kwamba kuna utata mkubwa juu ya namna Marekani itakavyojibu hatua hiyo. 

O'Brien alisema hapo jana akiwa mjini Nevada, Las Vegas, kwamba China inafanya matayarisho makubwa ya jeshi la majini ambayo yumkini hayajawahi kushuhudiwa tangu jaribio la Ujerumani kushindana na jeshi la majini la Uingereza kabla ya Vita Vikuu vya Kwanza vya Dunia. 


Alisema sehemu ya matayarisho hayo ni kuwapa uwezo wa kuisukuma Marekani nje ya Pasifiki Magharibi, na kuwaruhusu kutua Taiwan katika operesheni za jeshi la ardhini, baharini na angani. 


Marekani inatakiwa kisheria kuipaTaiwan uwezo wa kujilinda, lakini haijabainisha wazi iwapo itangilia kijeshi ikiwa China itaishambulia Taiwan, jambo ambalo huenda likasababisha mzozo mpana zaidi na Beijing. 


O'Brien pia ameitolea wito Taiwan kuongeza matumizi yake ya kijeshi na kufanya mageuzi ya kijeshi, ili kuipa ujumbe wa wazi China juu ya hatari za kujaribu kuivamia. China inaitambuwa Taiwan kuwa sehemu yake iliyojitenga.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad