Wanajeshi Nigeria wafyatua risasi dhidi ya waandamanaji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Watu wawili wamejeruhiwa hapo jana mjini Lagos, Nigeria, baada ya wanajeshi kuwafyatulia risasi za moto waandamanaji wanaopinga ukatili wa polisi, kulingana na mashuhuda.

Taarifa hizo ni kulingana na mashuhuda wanne waliozungumza na shirika la habari la Reuters. Jeshi la Nigeria hata hivyo limedai kuwa wanajeshi wake hawakuweko katika eneo hilo la maandamano JUmanne. Serikali imesema itafanya uchunguzi dhidi ya tukio hilo.


Aidha Jumanne kumetangazwa amri ya kutotembea usiku ya muda wa masaa 24 katika mji wa Lagos ambao ni kitovu cha biashara Nigeria, wakati vurugu zikiongezeka katika maandamano ambayo yametikisa miji kadhaa nchini humo.


Ni moja ya majimbo matatu kati ya 36 ya Nigeria yaliyotangaza hatua kama hiyo katika siku mbili zilizopita. Mkuu wa polisi wa kitaifa pia aliamuru kupelekwa mara moja kwa vikosi vya kupambana na ghasia kote nchini kufuatia kuongezeka kwa mashambulio kwenye vituo vya polisi, kulingana na msemaji wa polisi.


Shirika la kutetea haki za binadamu Amnesty International limesema lina ushahidi wa matumizi mabaya ya nguvu na kusababisha vifo vya waandamanaji, na kwamba takriban watu 15 wameuawa tangu maandamano hayo kuanza.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad