Biden: Trump kukataa kushindwa 'ni aibu'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Joe Biden amesema hatua ya Rais Donald Trump kukubali kushindwa katika uchaguzi wa urais wa wiki iliyopita ni "aibu".

Lakini rais huyo mteule wa Marekani- ambaye amekuwa akiwasiliana na viongozi wa kimataifa - amesisitiza kwamba hakuna kitu kitakachozuia uhamisho wa madaraka.


Huku hayo yakijiri Bw. Trump aliweka ujumbe kwenye mtandao wake wa Twitter akisema atashinda kinyang'anyiro hicho cha uchaguzi ambacho kilibashiriwa na vituo vikuu vya televisheni kwamba atashindwa.


Kama inavyofanyika kila miaka minne, vyombo vya habari vya Marekani hubashiri mshindi.


Mpaka sasa matokeo ya uchaguzi kutoka majimbo ya Marekani hayajaidhinishwa, kura bado zinahesabiwa, lakini matokeo yatatolewa rasmi wajumbe maalum watakapokutana Disemba, 14.


Biden amesema nini?


Rais mteule aliulizwa na waandishi wa habari siku ya Jumanne kile anachofikiria kuhusu hatua ya Rais Trump kukubali kwamba alishindwa kaika uchaguzi.


"Nadhani ni aibu, kusema kweli," Bw. Biden, mwanachama wa Democratic, alisema mjini Wilmington, Delaware.


"Kile ninachoweza kusema, kwa heshima, Nadhani hatua hiyo haitasaidia kudumisha hadhi ya rais atakapoondoka madarakani."


"Mwisho wa siku, mbivu na mbichi itajulikana Januari 20," alisema akiashiria siku ya kuapishwa.


Bw. Biden amekuwa akiwasiliana kwa njia ya simu na viongozi wa kigeni anapojiandaa kuingia rasmi ofisini.


Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson, Kiongozi wa Ireland Taoiseach Micheál Martin, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ni miongoni wa viongozi aliosema nao siku ya Jumanne.


Akiashiria mawasiliano hayo ya simu, Bw. Biden alisema: "Nawafahamisha kwamba Marekani imerejea tena ulingoni. Tunarudi tena katika nafasi yetu mchezoni."


Yeye na Makamu wa Rais mteule Kamala Harris wanaendelea mbele na mpango wa kuingia mamlakani. Lakini shirika dogo linaloongozwa na washirika wa Trump linadiwa kulemaza mpango huo.


Shirika hilo linalosimamia huduma zote za serikali kuu ikiwa ni pamoja na kufadhili na kusaidia utawala mpya unaoingia madarakani kufikia idara za serikali, mpaka sasa limekataa kumtambua rasmi Bw. Biden kama rais mteule.


Hata hivvyo, rais mteule amesema: "Hatuoni kitu chochote kikirudisha nyuma mipango yetu, kusema kweli."

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad