Chanjo ya Moderna inazuia Covid-19 kwa 95%

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Chanjo mpya inayozuia ugonjwa wa Covid-19 ina karibu 95% ya ufanisi , data kutoka Kampuni ya Marekani Moderna inaonesha,

Matokeo haya yamekuja sawa na yale ya chanjo ya Pfizer, na kuongeza imani kuwa chanjo zinaweza kusaidia kumaliza janga hili.


Kampuni zote mbili zilitumia mbinu na majaribio ya chanjo zao.


Moderna inasema hiyo ni "siku muhimu" na wanapanga kuomba idhini ya kutumia chanjo hiyo katika wiki chache zijazo.


Hatahivyo hizi ni data za awali , na maswali muhimu bado yamebaki yakiwa hayajajibiwa


Ni nzuri kiasi gani?


Jaribio hilo lilihusisha watu 30,000 huko Marekani na nusu wakipewa dozi mbili za chanjo, wiki nne tofauti. Wengine walikuwa na sindano .


Uchambuzi huo ulitokana na 95 wa kwanza waliokuwa na dalili za Covid-19.


Takwimu hizo pia zinaonesha kulikuwa na wagonjwa 11 wa Covid lakini hakuna hata mmoja aliyetokea kwa watu ambao walikuwa wamepewa chanjo.


"Ufanisi wa jumla umekuwa wa kushangaza ... ni siku nzuri," Tal Zaks, afisa mkuu wa tiba huko Moderna, aliambia BBC News.


Rais wa Kampuni hiyo Dkt Stephen Hoge aliiambia BBC News: "Sidhani kama yeyote kati yetu alitumai kweli kwamba chanjo hiyo itakuwa na ufanisi wa 94% katika kuzuia ugonjwa wa Covid-19, huo ulikuwa utambuzi mzuri sana."

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad