Malawi yamuachia Huru Nabii Milionea Aliyekiuka Masharti ya Dhamana Afrika Kusini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Nabii milionea wa Malawi Shepherd Bushiri na mke
wake wameachiwa bila masharti yoyote na mahakama moja mjini Lilongwe nchini Malawi baada ya kujisalimisha kwa polisi Jumatano.

Afrika Kusini inataka ikabidhiwe wawili hao kwa kukiuka masharti ya dhamani nchini humo.


Bushiri na mke wake wameshtakiwa nchini Afrika Kusini walikokuwa wanaishi kwa makosa ya utakatishaji wa fedha na ulaghai.


Hata hivyo wawili hao wamekanusha mashtaka hayo.


Wakili wao, Wapona Kita, aliitaka mahakama iwaachilie wawili hao bila masharti yoyote akisema kuwa kukamatwa kwao ni kinyume na sheria.


Mwendesha mashtaka aliomba mahakama kuruhusu polisi kuendelea kuwashikilia wanandoa hao kwa siku 30 zaidi ili kuwezesha Afrika Kusini kuwasilisha rasmi ombi lao la kutaka wakabidhiwe kwa nchi hiyo.


Bwana Kita alisema ni kinyume cha sheria kumzuilia mtu wakati Afrika Kusini haijawasilisha ombi rasmi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad