Mama Ahukumiwa Miaka Miwili Jela kwa Kumchana Mtoto na Wembe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mahakama ya Wilaya ya Kigoma mkoani Kigoma imemhukunu kwenda jela miaka miwili pamoja na faini ya Milioni 5, Agnes Damian(40) mkazi wa Mji Mwema Manispaa ya Kigoma Ujiji baada ya kupatikana na hatia ya kumchanachana na wembe sehemu mbalimbali za mwili Binti wa miaka 15 ambaye ni mtoto wa mume wake.


Hukumu hiyo imetolewa leo Novemba 30 na Hakimu, Eva Mushi ambaye amesema l adhabu hiyo inapaswa kuwa fundisho na onyo kwa wanaotenda matukio ya kikatili hasa kwa watoto.


Agnes anadaiwa kutenda tukio hilo Juni 18, ambapo aliingia chumbani nakufanya ukatili huo akimtuhumu kuwa Binti huyo alimpiga mwanae hivyo lazima ampe onyo.


Kabla ya adhabu hiyo, Agnes aliomba kupunguziwa adhabu kwakuwa anatunza watoto wawili, ni yatima na hivi karibu amepona ugonjwa wa kupoza japo hajawa timamu asilimia mia moja.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad