Wakenya waliokuwa wakielekea Dubai wakamatwa na satakabadhi gushi za corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Maafisa wa uwanja wa ndege nchini Kenya wamewakamata wasafiri 21 ambao waliokuwa wakielekea mjini Dubai, katika Muungano wa falme za kiarabu (UAE), kwa kutumia vyeti gushi vya Covid-19.

Wasafiri waliokamatwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.


Wasafiri hao wamekamatwa wakati wa msako wa vyeti hivyo uliokuwa ukifanyika katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta katika mji mkuu, Nairobi.


Hii inakuja saa kadhaa baada ya UAE kupiga marufuku utoaji wa vibali vya kusafiria (visa) kwa wasafiri wanaotoka nchi kadhaa ikiwa ni pamoja na Kenya.


Vyombo vya habari nchini Kenya vinaripoti kuwa marufuku hiyo iliwekwa baada ya wasafiri kutoka Kenya kupatikana na vyetu gushi vya Covid-19 walippowasili katika taifa hilo la Ghuba.


Kenya imekuwa ikirekodi ongezeko la maambukizi ya Covid-19, huku jumla ya watu wenye maambukizi ikifikia 80,102 vikiwemo vifo vya watu 1,427.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad