Chadema:Bado msimamo wetu ni ule ule,hatuwatambui madiwani na wabunge walioshinda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Na Amiri Kilagalila,Njombe

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema mkoa wa Njombe amesema Chama hicho kitaendelea kusimamia msimamo wao wa Chama wa kuto kuwatambua madiwani na wabunge waliochaguliwa kwenye nafasi zao mpaka pale utaratibu mwingine utakapotangazwa.



Bi,Rose Mayemba ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wetu juu ukimya wa uongozi wa Chama mkoa tangu ulipomalizika uchaguzi mkuu hapo Octoba 28 mwaka huu.



“Kama ambavyo katibu mkuu wa Chama chetu alivyozungumza juu ya wote walioshinda kwenye nafasi zao Chama hakijabadirika bado kwamba hawatambuliwi wabunge na hawatambuliwi madiwani, Tumezungumza na madiwani wetu wote wa kata nne kupitia makatibu wao wa wilaya na majimbo juu ya msimamo wa Chama na kama kuna mtu atakaidi nafikiri taratibu za Chama zitafuatwa” alisema Rose Mayemba mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Njombe



Aidha kuhusu ukimya wao mwenyekiti amesema ni kutokana na sintofahamu iliyokuwa imejitokeza wakati wa Uchaguzi kwa madai ya kugubikwa kwa vitendo visivyo kuwa vya huru na haki mpaka kutangazwa kwa ushindi katika uchaguzi huo.



 “Chadema mkoa wa Njombe tumekuwa kimya kwa muda mrefu tangu kufanyika kwa uchaguzi kwasababu ya sintofahamu iliyokuwa imetokea ambayo watanzania wote wanajua,Kwa muda kidogo tulikuwa kimya kwasababu Chama kilikuwa kwenye tafakari kubwa,na viongozi wetu wa Chama ngazi ya taifa wameshazungumza kuhusiana na uchaguzi na sisi bado tuko imara pengine zaidi ya ilivyokuwa”Alisema Rose Mayemba



Pia ameongeza “Imani ya watanzani kwa Chadema bado haijayumba iko pale pale katika kutafuta mabadiriko na tunaamini kila kitu kitakuwa sawa” Rose Mayemba

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad