Mlinzi wa Bobi Wine Adaiwa Kufa kwa Kugongwa Gari la Jeshi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



RIPOTI za vyombo vya habari nchini Uganda zimesema kuwa, baadhi ya mashahidi wameripoti kwamba mlinzi wa mgombea urais kupitia National Union Party (NUP), Robert Kyagulanyi Ssentamu ‘Bobi Wine’ aitwaye Francis Kalibala, aligongwa na gari la Jeshi la Uganda (UPDF) wakati msafara wa Bobi Wine upolikuwa unarudi Kampala kutoka Masaka.

 

Katika taarifa yake, Bobi Wine amesema, “Nasikitika kutangaza kifo cha mmoja wa walinzi wangu, Francis Kalibala, aliyegongwa na gari la jeshi, namba H4DF 2382 ambalo liliziba njia karibu na Busega na kutuzuia kupita.”


Msemaji wa Jeshi la Uganda, Brig. Flavia Byekwaso amesema, Francis alianguka kutoka kwenye gari lililokuwa linaendeshwa kwa mwendokasi.


Kabla ya tukio hilo, waandishi kadhaa wa habari walishambuliwa na polisi na kujeruhiwa vibaya akiwemo mpiga picha Ashraf Kasirye wa televisheni ya Bobi Wine ya Ghetto TV, na mwandishi wa Shirika la Habari la Nation Media Group – NTV, Ali Mivule.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad