Breaking: Mkurugenzi TPA Akamtwa na TAKUKURU

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





TAKUKURU inamshikilia kwa mahojiano Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko aliyesimamishwa kazi na Rais Samia Suluhu Hassan kwa tuhuma za ubadhirifu wa TZS bilioni 3.6. Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo amethibitisha.

 

 

“Kumshikilia mtu ni suala la kawaida kama kuna tatizo limetokea na kama mlivyomsikia Mhe. Rais amemsimamisha kazi kwa sababu ya matatizo na sisi ni kweli tunamshikilia ili tuweze kufanya uchunguzi vizuri,” amesema Mbungo.

 

 

Taarifa zinaeleza mmemshikilia akiwa anatoroka ni kweli?

“Hapana sisi hatuna huo ukweli wa kutoroka lakini tumemshikilia kwa sababu ambazo isingekuwa vyema mimi niziongee hapa sasa hivi, lakini ni utaratibu tu wa uchunguzi.” amesema Mbungo.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad