Daktari Scott Green ajiunga na kesi kupitia Zoom huku akimfanyia mgonjwa upasuaji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Daktari mmoja, katika jimbo la California alijiunga na kesi ya uvunjifu wa sheria barabarani kupitia mtandao wa Zoom huku akimfanyia mgonjwa upasuaji.
Scott Green aliyekuwa amevalia mavazi ya kufanya upasuaji, tayari alikuwa katika chumba cha upasuaji wakati alipojiunga na mahakama kusikiliza kesi dhidi yake mtandaoni siku ya Alhamisi, Sacramento Bee iliripoti.

Alipoulizwa na jaji, Bw. Green alisema anaweza kuendelea na kesi, na kuongeza yuko na "mpasuaji mwingine ambaye anashirikiana naye".

Jaji alisema haitakuwa "sawa" na kuahirisha kesi.

Bodi ya Matibabu ya California imesema katika taarifa kwamba inachunguza kisa hicho, ikiongeza kuwa "anatarajia madaktari kufuata kanuni ya huduma wakati wa kutibu wagonjwa wao".

Kabla ya kusikizwa kwa kesi mbele ya Mahakama ya Juu zaidi ya Sacramento, ambayo ilioneshwa mubashara katika mtandao wa YouTube, karani wa mahakama alimuuliza daktari huyo: "Hujambo, Bw Green? Salama. Unapatikana kushiriki kesi hii? Inaonekana kana kwamba upo katika chumba cha upasuaji."

Green alimjibu: "Naam ni mimi, mkuu. Ndio, Niko katika chumba cha upasuaji muda huu. Naam, naweza kushiriki kwenye kesi. Endelea mbele."

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad