Mtihani Mzito Penzi La Kajala, Harmo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Unawezakuwa mtihani wa kwanza kabisa kwenye mahusiano yao kama habari zilizolifikia gazeti hili zikiwa na ukweli wa asilimia mia.

Taarifa ikufikie kwamba, kuna madai kuwa penzi hili jipya la muigizaji Kajala Masanja na Rajabu Abdul ‘Harmonize’ limeingia ‘mushkeli’ kufuatia Kajala kuhoji juu ya tatuu aliyonayo Harmonize.

 

Tatuu hiyo si nyingine bali ni ile ambayo Harmonize amejichora kwenye mkono wake wa kuume ikisomeka ‘Sarah’ yaani yule mkewe waliyemwagana miezi kadhaa iliyopita, kabla ya kutua kwa Kajala.

“Yaani unaambiwa Kajala kamaindi sana kuhusu hiyo kitu lakini hata hivyo inaonekana Harmonize katumia uanaume wake kumuweka sawa.“

Amemwambia ni suala la muda tu tatuu hiyo ataangalia namna ya kuibadili isisomeke Sarah maana kuifuta kabisa ni ngumu,” alieleza mtu wa karibu na Kajala.

 



Mtu huyo alizidi kutanabaisha kuwa, Kajala amekuwa muelewa kwani tayari ni mtu mzima na anajua jinsi gani maisha ya mahusiano yalivyo.

“Unajua Kajala licha ya kumaindi lakini bado anarudi nyuma kidogo kifikra maana yeye sio mtoto mdogo.

Ameshakuwa na mahusiano tofauti kabla ya kuwa na Harmo.

 

Kajala si unakumbuka alishaolewa kabisa na akaachana na mumewe hivyo baada ya kuwekwa chini anaonekana kuelewa,” kilisema chanzo hicho.

 

Mtu huyo alisema, kwa jinsi Harmonize alivyokufa na kuoza kwa Kajala, yupo tayari kwa lolote kwani hataki kumpoteza hivyo jambo hilo atahakikisha linakwisha na kumpa furaha kama aliyokuwa nayo awali.

 

“Harmonize humwambii kitu kwa Kajala na ndio maana unaona ndani ya muda mfupi tu tayari ameshamnunulia Kajala gari na hata nyumba.“Harmonize yupo serious kwenye hili penzi kuliko watu wengi wanavyofikiria. Alimzimia kitambo sana Kajala sema tu alikosa nafasi ya kuwa wake,” kiliweka nukta chanzo hicho.



Jitihada za kuwapata wawili hao ambao kwa sasa penzi lao liko moto hazikuzaa matunda kufuatia simu zao kuita muda mrefu bila kupokelewa.Hata hivyo, jitihada zaidi zinaendelea na tunaamini watapatikana na kuweka kila kitu hadharani.

TUJIKUMBUSHE

Penzi la Kajala na Harmonize limechipuka hivi karibuni na kuzua gumzo sana kwenye mitandao hususan watu wengi kujadili suala la umri kwamba Kajala ni mkubwa zaidi ya Harmo.Hata hivyo wenyewe wameziba masikio na wameendeleza mahusiano yao kwa kuzunguka sehemu mbalimbali za starehe na kutupia mapicha kama yote kupitia kurasa zao za mtandao wa Instagram.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad