Msichana wa asili ya Kiafrika apigwa risasi na kuuawa na polisi Ohio, Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Maafisa wa polisi wameripotiwa kumuua msichana wa miaka 16 wa asili ya Kiafrika katika jimbo la Ohio la nchini Marekani (USA).

Polisi walichukua hatua mjini Columbus, Ohio, baada ya kupokea taarifa ya kuzuka kwa mapigano ya kisu.

Maafisa wa polisi ambao walikwenda eneo la tukio, waliwafyatulia risasi wasichana walipokuwa wakijaribu kutoroka.

Makiyah Bryant, msichana mwenye umri wa miaka 16 ambaye alipigwa na risasi, alifariki katika hospitali alikopelekwa licha ya juhudi za matibabu.

Polisi walitoa picha za kamera zilizorekodi tukio hilo.

Katika taarifa kwenye vyombo vya habari vya ndani ya nchi, ilisisitizwa kuwa Bryant alikuwa ameshika kisu mkononi mwake kujikinga na watu wazima waliomshambulia.

Hata hivyo, ilielezwa kuwa polisi waliacha kisu hicho walipofika eneo la hilo.

Familia ya Byrant pia ilisema kwamba polisi walimpiga risasi msichana huyo mdogo bila kumtahadharisha kwa onyo lolote.

Wakati uchunguzi wa tukio hilo ulianzishwa, waandamanaji waliingia barabarani tena kupinga vurugu za polisi baada ya mauaji.

Waandamanaji walikusanyika mbele ya makao makuu ya polisi mjini humo kupinga ghasia za polisi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad