AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kocha wa AS Vita Florent Ibenge amekiri kuwa kwasasa vilabu vya Tanzania vimeimarika kifedha ndio maana vinaweza kusajili wachezaji kutoka DR Congo kwenye vilabu vikubwa kama TP Mazembe na AS Vita.
Kauli hiyo ameitoa baada ya hizo za DRC kuondolewa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika huku Simba SC ya Tanzania ikifuzu robo fainali kwa kuongoza kundi A.
''Mpira wa sasa unahitaji pesa, na kwa sasa vilabu vya Tanzania vipo vizuri kwenye pesa ndio maana vinamudu kusajili wachezaji wenye uwezo mkubwa. Hata wachezaji wa DR Congo wenye viwango vya juu wanakimbilia Tanzania,'' amesema Ibenge.
Simba imefuzu robo fainali baada ya jana April 3, 2021 kuifunga AS Vita magoli 4-1 na kufikisha pointi 13 na kuongoza Kundi A lenye timu za Al Ahly, AS Vita na Al-Merrikh.
Mabingwa mara tano wa Ligi ya Mabingwa Afrika TP Mazembe nao pia wameondolewa katika hatua ya makundi.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK