Waziri wa afya wa Uingereza ajiuzulu kwa kuvunja sheria za corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Waziri wa afya wa Uingereza Matt Hancock amejiuzulu. Hancock amejiuzulu baada ya kuvunja sheria ya kuthibiti kuenea kwa virusi vya corona kwa kuweka umbali wa mtu mmoja hadi mwingine akiwa na msaidizi wake mkuu Gina Coladangelo anayedaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye. 
Gazeti la The Sun lilichapisha picha zilizoonekana kumuonesha Hancock na Coladangelo wakibusiana katika ofisi moja ya wizara hiyo ya afya. 

Katika barua yake ya kujiuzulu kwa waziri mkuu Boris Johnson, Hancock alisema kuwa serikali ina wajibu kwa watu wake ambao wamejitolea pakubwa katika janga la virusi vya corona, kuwa waaminifu kwao wakati imewakosea.

Hancock aliongeza kuwa anataka kusisitiza ombi lake la msamaha kwa kuvunja muongozo na kuiomba radhi familia na wapendwa wake kwa tukio hilo na kwamba anahitaji kuwa na watoto wake kwa wakati huu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad