Morrison Aondolewa Kikosini Simba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




KIUNGO Mshambuliaji wa Simba, Bernard Morrison, ameondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo kufuatia kuwa na matatizo ya kifamilia.

 

Morrison ambaye wikiendi iliyopita kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga ambao Simba walifungwa bao 1-0 alicheza dakika zote tisini, anatarajiwa kuukosa mch–ezo wa leo Jumapili dhidi ya Coastal Union utakaochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar.

 

Katika mazoezi ya jana Jumamosi yaliyofanyika Simba Mo Arena, Dar, na kushuhudiwa na Spoti Xtra, Morrison hakuwa sehemu ya mazoezi hayo ya mwisho kabla ya kuivaa Coastal Un–ion leo Jumapili.

 

Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu, alisema: “Morrison hayupo na timu kwa sababu ya matatizo ya kifamilia, pia kuna wachezaji wengine watakosekana katika mchezo dhidi ya Coastal akiwemo Parfect Chikwende ambaye yupo na kikosi cha timu yao ya taifa.”

STORI: CAREEN OSCAR,Dar es Salaam

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad