Mwanariadha Mjerumani mwenye asili ya Tanzania ashinda medali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Raia wa Ujerumani mwenye asili ya Tanzania Malaika Mihambo, amelishindia taifa lake medali ya dhahabu katika mashindano ya michezo ya Olimpiki ya long Jump.


Mwanaridha huyo aliruka urefu wa mita saba ili kuchukua ushindi.

Awali Mihambo alikabiliwa na changamoto kadhaa kabla ya mashindano hayo lakini hatimaye alifanikiwa kuonesha umahiri wake.

Katika fainali ya mchezo huo iliofanyika hii leo Jumanne, bi Malaika hakuonesha ishara zozote za kuibuka mshindi.

Urefu wa mita saba alioruka katika jaribio la sita ulimwezesha kuipatia Ujerumani nishani yake ya kwanza ya dhahabu katika mchezo huo tangu Heike Drechsler aliposhinda mwaka 2000.

Nishani ya fedha ilimwendea mshindi mara nne wa mashindano ya dunia na Olimpiki yaliofanyika mjini London Brittney Reese wa Marekani baada ya kuruka mita 6.97 huku Ese Brume wa Nigeria akijinyakulia medali ya shaba na kuiongezea Afrika idadi ya medali katika michezo hiyo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad