Roketi tano zarushwa kuelekea kwenye uwanja wa ndege wa Kabul

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Roketi kadhaa zilirushwa kuelekea kwenye Uwanja wa ndege wa Kabul mapema leo. Televisheni ya Tolo ya mji wa Kabul imewanukuu walioshuhudia shambulio hilo. 
 
Kwa mujibu wa taarifa makombora hayo yalirushwa kutokea mji wa Chairchanah uliopo kaskazini mwa mji wa Kabul. Hakuna madhara yaliyoripotiwa. 
 
Habari zaidi zinasema mfumo wa ulinzi wa anga ulikuwa umewekwa tayari. Maafisa wa serikali ya Marekani wamefahamisha kuwa mfumo huo ulifanyiwa majaribio wiki iliyopita. 
 
Shirika la televisheni la Marekani, CNN ,limeripoti kwamba hatari iliyokuwepo hapo awali ya uwanja wa ndege wa Kabul kushambuliwa sasa imeondolewa. 
 
Marekani imekamilisha shughuli za kuwaondoa watu na wanajeshi wake wanatarajiwa kuondoka Kabul hapo kesho Jumanne. 
 
Watu wapatao 114,000 wamesafirishwa kwa ndege kutoka Afghanistan tangu katikati ya mwezi Agosti, kulingana na Ikulu ya Marekani.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad