Mawakili wa Mbowe, wenzake wajigawa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



 

MAHAKAMA Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar es Salaam, imekubali ombi la mawakili wa utetezi katika   kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, la kujigawa katikati ya usikilizwaji wa kesi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Ombi hilo limekubaliwa Leo Ijumaa, tarehe 17 Septemba 2021, na mahakama hiyo mbele ya Jaji Siyani baada ya kiongozi wa Jopo la mawakili wa utetezi katika kesi hiyo, Peter Kibatala, kuiomba mahakama hiyo ikubali wajigawe.

Awali, Wakili Kibatala,  amedai kwamba wameamua kujigawa baada ya kubaini maelezo ya onyo ya mshtakiwa wa pili, Adam Kasekwa yana mgongano wa kimaslahi, akidai yalikuwa yanaelekea kuwataja washtakiwa wenzake.

Wakili Kibatala alidai makamani hapo kuwa, awali mawakili upande wa utetezi walikuwa wanawakilisha washtakiwa wote wanne pamoja, hivyo sasa wanaiomba mahakama hiyo ikubali mawakili hao wajigawe.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad