Mwanahabari Kivuyo Atambulishwa Kuwa Msemaji wa Geita Gold FC Iliyopanda Ligi Kuu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



MKURUGENZI wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Mhe. Zahara Michuzi amemtambulisha Mwanahabari mbobezi na mwandamizi katika maswala ya soka, Hemedy Kivuyo kuwa Msemaji Mkuu wa timu hiyo wakati Kikosi chao kikijiandaa na Ligi Kuu Soka Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la ASFC msimu wa 2021-2022.

Kivuyo ametambulishwa leo katika Tamasha la Geita Gol Day 2021 sambamba na kutambulishwa Wachezaji wapya watakaotumikia timu hiyo kwenye msimu huu wa mashindano.

Akizungumza kwenye tamasha hilo, Mhe. Zahara amesema ni rasmi Kivuyo atakuwa Msemaji wa Mabingwa na matajiri wa dhahabu (GGFC) wakati tukijiandaa kucheza Ligi Kuu na Mashindano mengine hapa nchini.

“Karibu sana kwenye familia ya Mabingwa Mr. Hemedy Kivuyo, Wanageita wana imani kubwa na wewe na wasubiri makubwa toka kwako”, ameeleza.

Kikosi cha Geita Gold FC kinachonolewa na Kocha Mkuu Etienne Ndayiragije kimepanda Ligi Kuu msimu huu wa mashindano wa 2021-2022 kwa mara ya kwanza wakitokea Ligi daraja la kwanza ambayo kwa sasa itatambulika kama Championship.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad