Rais Samia Suluhu Afanya Uteuzi wa Viongozi Mbalimbali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu 100 wauwawa katika shambulio la bomu Afghanistan

   Muungwana Blog 2        Oct 8, 2021

 





Mashambulizi katika msikiti mmoja wa kaskazini mwa Afghanistan, yaliyowalenga waumini wa Kiislamu wa madhehebu ya Shia, yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 100 huku wengine kadhaa wakijeruhiwa. 

Bomu liliripuka katika msikiti wa Gozar-e-Sayed Abad wakati wa sala ya Ijumaa. Ali Reza mmoja ya walioshuhudia tukio hilo amesema alikuwa anaswali wakati wa mripuko na ameripoti kuona majeruhi wengi. 

Picha na vidio za matukio zimeonyesha waokoaji wakibeba miili iliyokuwa imefungwa ndani ya blanketi kutoka msikitini hadi katika gari la kubebea wagonjwa. 

Ngazi za kuingilia msikiti huo zote zilikuwa zimejaa damu. 

Naibu polisi wa mkoa wa Kunduz, Dost Mohammad Obaida, amesema hakuna kundi lolote hadi sasa lililokiri kuhusika na shambulio hilo lakini wanamgambo wa kundi la dola la Kiislamu wana historia ya muda mrefu ya kuwashambulia waumini walio wachache wa Shia.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad