AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kundi la Taliban limeitaka Marekani kusikiliza wito uliotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres wa kuziachilia fedha za Afghanistan zilizoko Marekani, wakati ambapo mzozo wa kibinaadamu ukiongezeka.
Maafisa wa Marekani walizuia mali za Afghanistan zenye thamani ya mabilioni ya dola, baada ya kundi hilo lenye itikadi kali kuchukua madaraka mwezi Agosti baada ya kuondoka kwa majeshi ya kigeni.
Jana, Guterres aliitaka Marekani kuongoza katika kuzuia mzozo wa kiutu unaojitokeza Afghnistan kwa kuziachilia fedha hizo.
Waziri Bashungwa atoa maagizo kwa maaafis wa elimu
Msemaji wa serikali ya Taliban, Zabinullah Mujahid amesema Marekani inapaswa kuitikia vyema sauti ya kimataifa na kuziachia fedha hizo.
Marekani imechukua udhibiti wa takribani dola bilioni 9.5 ambazo ni mali ya Benki Kuu ya Afghanistan.
Hata hivyo Mashirika ya misaada na Umoja wa Mataifa yamekadiria kuwa zaidi ya nusu ya watu milioni 38 wa Afghanistan wanatarajiwa kukumbwa na njaa katika msimu huu wa baridi.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK