Dk Mwinyi Atengua Uteuzi wa Viongozi Watano

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Unguja. Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ametengua uteuzi wa viongozi katika Wizara za elimu, Uchumi na Uwekezaji na wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Katibu Mkuu Mtendaji, Zena Said leo Februari 3, 2022 imewataja waliotenguliwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Utumishi na Uendeshaji Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Omar Ali Omar.

Mwingine aliyetajwa katika taarifa hiyo ni Suleiman Yahya Ame Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu katika wizara hiyo ya elimu.

Wengine ni Fatma Iddi Ali, Kamishna wa Kazi katika ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji na Salum Ubwa Nassor, Ofisa Mdhamini, Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo, Pemba.


Katika orodha hiyo pia kuna Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia na Watoto katika Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto, Nasima Haji Choum

Ametengua nafasi hizo kuanzia leo
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad