TMA yatoa angalizo mvua kubwa na upepo mkali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo kwa wananchi juu ya hali ya hewa katika siku kadhaa zijazo.
JUMAPILI 06-02-2022

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Iringa, Njombe, Songwe, Mbeya, Ruvuma Lindi na Mtwara.
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.

KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI.

JUMATATU 07-02-2022

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa maeneo machache ya mikoa ya Dodoma, Morogoro, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa, Ruvuma Lindi na Mtwara.

ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2.0 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya bahari ya Hindi mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.
KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI.


 
JUMANNE 08-02-2022

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Lindi na Mtwara.

ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2.0 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya bahari ya Hindi mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.
KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI.

JUMATANO 09-02-2022
ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2.0 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya bahari ya Hindi (mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam na Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba).
UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI.


Utabiri huu umetolewa,
Na, MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad