Abramovic wa Chelsea Awachanganya Mashabiki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



BILIONEA Roman Abramovich ametoa ujumbe unaoonyesha kuwa amejiuzulu kuimiliki Chelsea lakini bado ujumbe huo hauko wazi sana.

Hiyo ni baada ya Mrusi huyo kuonekana kuwa na ukaribu na Rais wa Urusi, Vladimir Putin ambaye majeshi yake yameleta vita kwa kuivamia Ukraine.

Mmiliki huyo aliyeinunua Chelsea Julai 2003, alitoa ujumbe kama wa kujiuzulu kwenye tovuti ya klabu hiyo juzi usiku.

Abramovich aliandika: “Wakati wa karibu miaka 20 ya umiliki wangu wa Chelsea FC, daima nimekuwa nikitathmini wajibu wangu kama kiongozi wa klabu, ambaye kazi yake ni kuhakikisha tuna mafanikio, pamoja na kujenga kwa ajili ya siku zijazo, huku pia tukiwa na msaada kwenye jamii.


“Daima nimekuwa nikifanya maamuzi kwa faida ya klabu. Bado ninasimamia misingi hii.

“Ndiyo maana leo ninatoa kwa wengine umiliki wa Taasisi ya Misaada ya Chelsea na uangalizi wa Chelsea FC. Ninaamini (watakaochukua nafasi) kwa sasa wapo katika nafasi nzuri ya kuangalia ubora wa klabu, wachezaji, wafanyakazi na mashabiki.”

Baada ya tamko hilo, mashabiki wa Chelsea wamechanganywa wakiwa hawajui kama ndio ameachia ngazi moja kwa moja au la.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad