ELIZABETH Michael almaarufu Lulu Afunguka Issue ya Kumnyonyesha Mwanae

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


ELIZABETH Michael almaarufu Lulu au Mama G; ni supastaa filamu za Kibongo tangu akiwa na umri wa miaka mitano ambaye mwaka jana alijaaliwa mwanawe wa kwanza kwa mumewe, Francis Ciza almaafu DJ Majizzo.

Lulu au Lizy anasema kuwa, baada ya Mungu kumjaalia mtoto huyo aliyempa jina la Genesis atamnyonyesha hadi afikishe umri wa mwisho wa kumuachisha nyonyo na siyo kumuachisha tu, kisa kutaka usichana.

Akizungumza na Gazeti la IJUMAA, Lulu anasema kuwa, mastaa wengi wanaogopa kunyonyesha wakihofia maumbo yao kuharibika, lakini kwa upande wake hakuna cha kuhofia kwa sababu anatafuta afya njema kwa mtoto wake na siyo kitu kingine.

“Nitamnyonyesha hadi inapotakiwa, mambo ya kuhofia mwili wangu kuharibika siyo kweli kabisa, watu wanyonyeshe, mimi mambo ya kujihofia mwili wangu sitaki kwa sababu ukweli ni kwamba mimi ni mama na hakuna cha kubadilisha,” anasema Lulu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad