Kenya Yaorodheshwa ya 5 katika Orodha ya Nchi Tajiri Zaidi Barani Afrika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Kenya Yaorodheshwa ya 5 katika Orodha ya Nchi Tajiri Zaidi Barani Afrika
Kenya Yaorodheshwa ya 5 katika Orodha ya Nchi Tajiri Zaidi Barani Afrika.
Ripoti ya Africa Wealth ya New World Wealth and Henley & Partners inaonyesha kwamba watu hao ambao hawakutajwa majina wana thamani ya zaidi ya $1 milioni, au KSh 115 milioni.

Ripoti hiyo iliorodhesha Afrika Kusini ikiwa na watu 39,300 wenye thamani ya juu (HNWI), ikifuatiwa na Misri yenye watu 16,900, Nigeria ikiwa na 10,000 na Morocco yenye matajiri 5,000.

"Nchi kubwa zina faida dhahiri kwa sababu ya idadi kubwa ya watu. Kama inavyoonekana, soko la utajiri la ‘Big 5’ barani Afrika ni Afrika Kusini, Misri, Nigeria, Morocco na Kenya – kwa pamoja, nchi hizi tano zinachukua zaidi ya asilimia 50 ya utajiri wote wa Afrika,” ripoti hiyo ilibainisha.


 
"Kwa hakika, Afrika Kusini ina mamilionea zaidi ya mara mbili ya nchi nyingine yoyote ya Afrika, wakati Misri ina mabilionea wengi zaidi barani."

Mabwenyenye
Utafiti huo pia unaonyesha kuwa kuna mamilionea wachache wa dola katika bara Afika.

Kulingana na ripoti hiyo, tajiri wa mamilioni ana thamani ya zaidi ya $10 milioni au KSh 1.16 bilioni, na kuna watu 340 tu kama hao nchini Kenya.


Afrika Kusini inaongoza na mamilionea wengi zaidi ya 2,080, ikifuatiwa na Misri yenye 880, Nigeria yenye watu 510, Morocco yenye 220 na Kenya yenye watu 340.

Masentimilionea wenye thamani ya zaidi ya $100 milioni au KSh 11.5 bilioni, wako 15 pekee nchini Kenya na 259 barani Afrika.

Kwa mara nyingine, Afrika Kusini inaongoza kwa 94, ikifuatiwa na Misri yenye 57, Nigeria 28, Morocco 22 na Kenya 15.

Kwa ujumla, ripoti hiyo iligundua kuwa hakuna bilionea wa dola nchini Kenya ambao ni 21 pekee barani Afrika.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad