Kijana Afikishwa Mahakamani Kwa Tuhuma za Kukata Viuno Hadharani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Maulid Hussein Abdallah, mkazi wa Kijiji cha Mwera Wilaya ya Magharibi Unguja visiwani Zanzibar, amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kukata viuno hadharani.

Kijana huyo anatuhumiwa kutenda kosa hilo katika Mji wa Kibole, Wilaya
ya Kati, Kusini Unguja majira ya saa 11 jioni ambapo inaelezwa kwamba akiwa amevalia mtandio, alianza kucheza kwa kukata viuno hadharani, jambo ambalo ni kosa la kisheria visiwani humo.

Mshitakiwa huyo amepinga mashtaka hayo na kuiomba mahakama kumpa
dhamana kwa kuwa yupo kituo cha polisi siku nyingi.

Amri ya kupelekwa rumande imetolewa na Hakimu Safia Waziri, baada ya
mshitakiwa kushindwa kutekeleza masharti ya dhamana ambayo yalimtaka kuwa na mdhamini mmoja ambaye atasaini bondi ya TZS 100,000 pamoja na barua zikiambatana na kopi ya kitambulisho cha Mzanzibar.

Mshitakiwa baada ya kushindwa kutekeleza masharti hayo, mahakama iliamuru arudishwe mahabusu hadi Aprili 25, mwaka huu kwa ajili ya kuanza
kusikiliza ushahidi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad