Breaking News: Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Yamsimamisha Mbatia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, imemsimamisha Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia na sekretarieti yake yote, kutojihusisha na siasa ndani ya chama hicho hadi uamuzi huo utakapoamuliwa vinginevyo.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Mei 25, 2022 na Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza akisema uamuzi wa Kikao cha Halmashauri ya chama hicho kilichofanyika Mei 21 mwaka huu, ulikuwa halali kwa akidi ya wajumbe wake licha ya kutotaja uhalali wa akidi hiyo.

Nyahoza amesema kwa mamlaka ya ofisi hiyo, inamtaka Mbatia kutojihusisha na siasa ndani ya chama hicho hadi uamuzi huo utakapotenguliwa na chama.


Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza
“Baada ya kusimamishwa, katibu wa chama hicho alituletea barua kwa fomu ya kisheria inayotujulisha kusimamishwa uanachama, tumekubaliana na uamuzi huo.


 
“Kama hawataridhika (Kina Mbatia) ziko njia za kutafuta haki, waende Mahakamani,” amesema Nyahoza.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad