Mwamuzi mwanamke kutoka Rwanda Salima Mukansanga kuchezesha kombe la Dunia Qatar 2022

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mwamuzi kutoka Rwanda, Salima Mukansanga ametajwa kuwa mmoja wa waamuzi watatu wa kike watakaochezesha Fainali za Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar.

Waamuzi wanamke hawajawahi kushiriki katika mashindano ya wanaume, kwa hivyo hii itakuwa ya kwanza kwenye mashindano mnamo Novemba.

Mukansanga amekuwa mwanamke wa kwanza kuchukua jukumu la mechi ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wanaume mapema mwaka huu

Kuna maafisa wengine kadhaa wa Kiafrika waliotajwa kwenda Qatar, akiwemo Janny Sikazwe, ambaye alivuma kwa kumaliza mechi sekunde 13 mapema katika mchezo wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwezi Januari.

Mapema leo kamati ya Waamuzi ya FIFA ilitangaza orodha yenye majina ya wasimamizi wa mechi waliochaguliwa kwa ajili ya Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022™.

Waamuzi 36, waamuzi wasaidizi 69 na maafisa 24 wa mechi za video wamechaguliwa kwa ushirikiano wa karibu na mashirikisho sita, kulingana na ubora wao na uchezaji uliotolewa kwenye mashindano ya FIFA na pia katika mashindano mengine ya kimataifa na ya nyumbani katika miaka ya hivi karibuni.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad