Bodi ya Ligi Wafunguka "Kanuni zitaamua mfungaji bora Endapo Mayele na George Mpole Wakilingana"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Bodi ya Ligi Tanzania Bara ‘TPLB’ imetoa ufafanuzi wa tuzo ya Mfungaji Bora kwa msimu wa 2021/22, ambao utafikia tamati leo Jumatano (Juni 29) katika viwanja vinane tofauti.


Hadi sasa Mshambuliaji wa Mabingwa Young Africans Fiston Kalala Mayele na George Mpole wanaendelea kupambana kuwania tuzo hiyo, huku kila mmoja akifunga mabao 16.


Afisa Habari wa TPLB Karim Boimanda, amesema endapo wawili hao watamaliza msimu wakiwa na mabao sawa ya kufunga, wataangalia kanuni ambazo zinatoa ufafanuzi nani anapaswa kuwa mfungaji bora.


Boimanda amesema: Ikitokea Fiston Mayele na George Mpole watamaliza msimu na magoli kama yalivyo sasa (16), kikanuni Mayele ndiye atakuwa mfungaji bora kwa kuwa hana goli la penati wakati Mpole ana penati mbili.”


Young Africans itamaliza msimu wa Ligi Kuu 2021/22 kwa kucheza didi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam, huku Mshambuliaji Fiston Mayele akitarajiwa kuwa sehemu ya kikosi cha klabu hiyo iliyotwaa Ubingwa wa Tanzana Bara.


Geita Gold FC nayo itamaliza msimu kwa kucheza dhidi ya Coastal Union katika Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga, huku George Mpole akitarajiwa kuwa sehemu ya kikosi cha Kocha Fred Felix Minziro.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad