Irene Uwoya Atoboa SIRI ya Kutozeeka Unaambiwa ni Kama JLO na Kim Kardashian

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Irene Pancras Uwoya; ni staa nembo wa Bongo Movies na ni mwanamama mjasiraiamali maarufu nchini Tanzania ambaye ametoa siri ya kutozeeka kwake na kuzidi kuonekana kabinti kabichi, IJUMAA lina exclusive.

Kumekuwa na mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii juu ya uzuri wa Uwoya mwenye umri wa miaka 33, akielezwa kuwa baadhi ya watu hukataa kwamba ni mama wa mtoto mmoja wa kiume, Krish Ndikumana.

Hii ni kutokana na kuendelea kuwa ‘kinanda’ zaidi kila kukicha.

KAMA JLO NA KIM

Wengine wanasema kuwa, huwenda Uwoya anatumia dozi ya kutozeeka kama akina Jeniffer Lopez (JLO) na Kim Kardshian wa Marekani.

Wengine wanadai kuwa huwenda Uwoya amefanya sajari ya ngozi ili kuonekana ya mtoto huku wengine wakidai kwamba, ni kwa sababu anaogea maziwa ya ng’ombe!

Wengine wanasema kuwa, Uwoya ni muigizaji ambaye watu wanatamani kumuangalia kuliko kuliko hata filamu yenyewe anayoigiza.

UKIKUTANA NAYE LAIVU SASA

Wengine wanasema kuwa, Uwoya anavutia kumtazama runingani, lakini ukikutana naye ‘laivu’ utaamini kuwa kamera zina chuki naye, kwani ni mzuri maradufu ya yule unayemuna runingani.

Sasa; mbali na runingani, Uwoya ni habari nyingine kwenye mitandaoni mitandao ya kijamii.

Uwoya akipsoti picha mpya, hadi wasanii wenzake na watu wake wa karibu akiwemo Aristote na Shamsa Ford, wanavutiwa naye na kummwagia sifa kedekede.

Wapo wanaosema kuwa, filamu inaweza kuwa mbaya, lakini wakijua Uwoya yumo ndani, basi watajilazimisha kuitazama ilimradi tu wamuone na siyo kujua stori ya filamu husika.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad