Manara: Kwenye Kikosi Bora cha Mwaka Yanga Tutaingiza Wachezaji 7-9, Morrison Ndani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Msemaji wa Yanga Haji Manara
MSEMAJI wa Klabu ya Yanga Haji Manara amesema kuwa kulingana na mafanikio waliyokuwa nayo klabu ya Yanga msimu huu kikosi bora cha msimu kwa mtazamo wake kinatakiwa kiwe na wachezaji zaidi ya 7 hadi 9.

Manara ameongea hayo kuelekea mchezo wa timu yake dhidi ya Coastal Union unaotarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam majira ya saa 2:30 usiku.

Msemaji huyo ameongezea kwa kusema kuwa mchezaji wa Simba Bernard Morrison naye anastahili kuwemo kwenye kikosi hicho licha ya kucheza michezo michache ya Ligi Kuu ya NBC msimu huu.


Kikosi cha Yanga
Alipoulizwa kwanini Bernard Morrison, wakati amecheza michezo michache? Manara alijibu kuwa Bernard Morrison ni mchezaji mwenye kipaji cha kipekee na ubora mkubwa unaomfanya aingie kwenye kikosi hicho.


 
Yanga itaingia uwanjani huku ikitarajiwa kukosa huduma ya nyota watatu Bakari Mwamnyeto ambaye ni majeruhi, Djigui Diarra ambaye hajapata mazoezi ya kutosha kutokana na kuwasili nchini muda si mrefu akitokea nyumbani kwao Mali pamoja na Kibwana Shomari ambaye ana jumla ya kadi tatu za njano.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad