AIBU: Bondia Mandoga Mtu Kazi Apingwa Tena KTO Afunguka "Hii ni Kama Ajali"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Bondia mwenye tambo na maneno mengi kutoka Mkoani Morogoro, Karim Mandonga kwa mara nyingine amechezea kichapo katika pambano la "Usiku wa Kisasi" dhidi ya Shabani Kaoneka pambano lililopigwa usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Majimaji Songea.


Pambano hilo la Mandonga ambalo lilikuwa pambano la utangulizi lilijipatia umaarufu mkubwa na kusubiriwa kwa hamu na wapenzi wafuatiliaji, limewastaajabisha watu wengi kutokana na matokeo yake kwani Mandonga alipigwa kwa TKO katika raundi ya nne dhidi ya Shabani Kaoneka.


Akizungumza baada ya Pambano mandonga alisema; "Hii ni kama ajali kazini, mtu anayependa kazi na asiyependa ajali inamkuta, lakini simuhofii Shaban Kaoneka, naweza sema pia ni mipango ya Mungu amepanga nipoteze na mimi sina uwezo wa kumbishia Mungu."- Mandonga aliiambia Azam TV.


Itakumbukwa, Mandonga amejipatia umaarufu mkubwa nchini licha ya kupoteza mapambano yake mawili mfululizo yaliyopita kutokana na kujiamini pamoja na tambo zake anazozionesha kabla ya mapambano yake.


Neno moja kwa Mandonga MTU kazi

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad