Serikali yaiagiza TARURA Kuvunja Mkataba na Mkandarasi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Serikali imeagiza Wakala wa barabara mjini na Vijijini (TARURA), Mkoa wa Singida kuvunja mkataba baina yao na Mkandarasi wa Kampuni ya Bullem Investment limited, wanaojenga Barabara ya kutoka Kitongoji cha Majengo hadi Hospitali ya wilaya kutokana na kushindwa kukamilisha kazi hiyo kwa wakati.


Agizo hilo limetolewa na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa Wilayani Manyoni, baada ya kupata malalamiko ya wananchi wa maeneo hayo waliomueleza kushindwa kukamilika kwa Barabara hiyo kwa kipindi kirefu na kusababisha usumbufu kwa wakazi wa eneo hilo.


Waziri Mkuu pia, amemuagiza Meneja TARURA Mkoa wa Singida kukagua na kumlipa Mkandarasi kulingana na asilimia zilizofikiwa katika Ujenzi wa Barabara hiyo, na asilimia zilizobaki apatiwe Makandarasi mwingine atakayeweza kukamilisha kazi hiyo kwa wakati.


Aidha, kutokana na kutokamilika kwa miradi mbalimbali Wilayani Manyoni ikiwemo mpango wa wamachinga, ujenzi wa soko na kutosikiliza na kutatua changamoto za wakazi, Waziri Mkuu amewahakikishi wananchi hao kuwa viongozi walihusika kukwamisha miradi ya Serikali watachukuliwa hatua za kinidhamu.


Wananchi hao, pia walilalamikia kutozwa fedha wakati wa kujifungua kina mama wajawazito, ukosefu wa masoko na huduma isiyoridhisha wa stendi ya mabasi na madeni ya fidia ya ardhi ya wananchi kitu ambacho kinawapa wakati mgumu.


Hata hivyo Waziri Mkuu amewaahidi wananchi hao kushughulikia suala la madeni ya fidia za ardhi, pamoja na changamoto ya Kodi huku akimtaka Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bilinith Mahenge kuhakikisha anarudi kuwasikiliza wafanyabiashara wadogo na kutatua changamoto zinazowakabili.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad