Nandy Aanika Vituko Vinavyotokana na Ujauzito Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




MSANII maarufu nchini Tanzania Nandy ameelezea kwa uwazi vituko anavyofanya kutokana na hali yake ya ujauzito. Anaripoti Juliana Assenga, UDSM … (endelea).

Nandy amefunguka na kusema toka apate ujauzito amekuwa hawapendi marafiki wa mume wake, na kupelekea kutoelewana nao, pia anasema nyakati zingine amekuwa hata akipokea simu zake na kuongea nao.

Msanii huyu pia anadai kuwa amekuwa akikwazika na kulia sana kiasi cha hata kumpelekea kutokula kwa siku mbili. Anasema amekuwa hivo hasa pale anaposemwa kidogo na mtu anaposhindwa kujirudi na kumuomba msamaha.

Nandy ambaye alikuwa akihojiwa katika kituo cha televisheni cha Wasafi amesema toka awe mjamzito amekuwa akipendelea kula chips maarufu kama Chips za Dubai mida ya saa 9 usiku.


Anasema kuwa hupendelea kula chips hizo kila ahisipo njaa na kuwa anaweza kuzila mara nyingi kwa siku hata akiwa amekwisha kula chakula cha jioni.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad