Binti Aliyepooza Mwili Mzima Abakwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mwanaume mmoja anayefahamika kwa jina la Juma Ligamba (45), mkazi wa Kijiji cha Kibubwa, Kata ya Butuguri wilayani Butiama mkoani Mara anadaiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka 19 ambaye ni mlemavu aliyepooza mwili mzima tangu kuzaliwa kwake.

Akisimulia kwa masikitiko tukio hilo la kubakwa kwa binti yake mama mzazi wa mtoto huyo anasema binti yake ana ulemavu huo unaomfanya muda wote kulala tu kwani alipooza mwili akiwa na wiki tatu tangu alipozaliwa kwake.

Nae Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Butiama, Devotha Paschal, amesema kwa kipindi cha hivi karibuni kumekuwepo na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wilayani humo huku mwanaasheria kutoka asasi isiyo ya kiserikali ya ATFGM Masanga Irene Assey, akikemea vikali juu ya vitendo hivyo vya ubakaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibubwa anasema alipata taarifa ya tukio hilo la ubakaji na kushirikiana na familia katika kumkamata mhalifu ambaye yupo chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi kwa sasa na uchunguzi unaendelea.


Naye, Adventina Victor ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya amekiri kumpokea mwathirika wa tukio hilo aliyefikishwa hospitalini hapo baada ya tukio hilo la kikatili na kusema kuwa anaendelea na matibabu.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad