Watanzania 33,000 hufa kwa moshi wa kupikia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Wastani wa Watanzania 33,000 hufariki kila mwaka, kutokana na moshi wa kupikia.

Waziri wa Nishati January Makamba alisema hayo jana jijini Dodoma, wakati wa semina ya kuwajengea uwezo Wabunge wanawake kuhusu matumizi ya nishati mbadala nyumbani.

Makamba ambaye yuko nje ya nchi kikazi, alitoa ujumbe huo mbao ulirekidiwa kabla ya kusafiri.

“Nilitamani kuhudhuria semina hii, lakini nimepata safari niko nje ya nchi, lakini kabla sijaondoka nilisema nitaacha rekodi ya ujumbe wangu,” alisema.


Alisema kuwa wastani wa Watanzania 33,000 wanakufa kila mwaka, kutokana na moshi wa kupikia kwa kuugua magonjwa ya mfumo wa hewa.

Alisema matumizi ya nishati mbadala yataokoa maisha ya kinamama na wote wanaotumia kuni.

“Saa moja kwenye jiko lenye moshi ni sawa na kuvuta sigara 300, ukimpima mwanamke wa Kijijini kwa X-ray ni kama mtu aliyevuta sigara muda mrefu, ule moshi ambao ni sumu unaofanya hata wadudu wasikae jikoni ndio unaingia kwenye mapafu,” alisema.


Alisema kuwa hiyo inonesha wanawake Tanzania wanameza moshi unaowaua taratibu.

” Madhara mengine ni watoto kuzaliwa njiti na mimba zinazotoka, ule moshi wa kupikia madhara yake hayazunguzwi sana, tunatakiwa kuchukua hatua. zinazostahili katika kumkomboa na kumsaidia mwanamke,” alisema.

Naibu Spika, Mussa Zungu alisema kuwa, matumizi ya kuni yamekuwa na madhara makubwa.

“Mlima Kilimanjaro unapoteza barafu kutokana na miti kukatwa, milima ikiishiwa barafu hakutakuwa na utalii tena,” alisema.


Mkurugenzi wa Masoko na Uendelezaji wa Teknolojia, Mhandisi Advera Mwijage, alisema kuwa wanahamasisha matumizi ya nishati vijijini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad