Binti wa Raila Odinga Winnie, adai kunyanyaswa kisa jina la baba yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Winnie Odinga, binti wa kiongozi wa upinzani wa Kenya Raila Odinga, amesema jina lake la familia limemfanya “kunyanyaswa” na “kuteswa” na halikuwa faida ya kisiasa kama wanavyodai baadhi ya wakosoaji.


Winnie Odinga, ambaye anawania kuwa mjumbe wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), alipinga wazo hilo katika kituo cha Citizen TV Kenyakwamba uhusiano wa familia yake ulikuwa nyuma ya uteuzi wake.


Bi Odinga alidai kuwa wakosoaji “hawataki kuangazia ninachoweza kufanya” kwa sababu ya babake ni nani.


Hata hivyo, alikubali kwamba jina la familia yake pia lilikuwa “baraka” ambayo imemruhusu kusafiri ulimwengu na kuelewa jinsi bara la Afrika linaweza kufanya kazi pamoja.


EALA ni chombo cha kutunga sheria cha jumuiya ya kikanda baina ya serikali, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na wanachama wanawakilisha mataifa yao kwa muhula wa miaka mitano.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad