Huyu Ndio Sarah Sadiki Alliyeacha Maumivu Makali kwenye Moyo wa Diamond Platnumz

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

Diamondplatnumz wakati amepakia post yake Instagram akitambulisha wimbo wake mpya wa #yatapita uliotoka siku ya Jana January 19/2023, amewausia wanawake wengi ambao wapo na wapenzi wao hivi sasa na maisha yao bado hayaeleweki kwa upande wao, kutowakimbia Wanaume wao kwa sababu za kiuchumi, wakafanya kama alivyo fanyiwa yeye na mpenzi wake aliyekuwa akiitwa SARAH.

Sarah ni nani? Wengi wameunganisha picha wakihisi anaye zungumziwa hapa ni Sarah wa #Harmonize , Lahasha! Huyu ni Sarah Sadiki mpenzi wa Zamani wa Diamond kabla ya kuwa staa, Diamond amewahi mzungumzia mara nyingi sana kwenye interviews za mwanzoni wakati anaanza kujulikana kwenye muziki, kama mwanamke aliyekuwa akimpenda sana ila bahati mbaya hakuwa mstahimilivu wa ahadi za matumaini zilizokuwa haziishi kutoka kwa Diamond.

NENDA KAMWAMBIE ni moja ya wimbo uliomtambulisha Diamond kwa ukubwa kwenye game ya Bongo Flava, na nyuma ya mashairi yenye hisia kali ya wimbo huo, kulikuwa na kumbukumbu za maumivu ya mapenzi kifuani kwa Diamond yaliyo achwa na Sarah kama kovu linalodumu juu ya ngozi ya mwanadamu katika maisha yake yote, Hivyo Nenda Kamwambie ilitungwa mahususi kwaajili ya mwanamke huyo.

Kabla ya Nenda kamwambie Diamond aliwahi fanya nyimbo kadhaa kama Rapa (2008), na Queen Darleen kiplay part kubwa ya kujaribu kumkutanisha Diamond na wasanii wakubwa kwa wakati huo kama Mr. Blue, Marehemu Albert Mangwair na Geez Mabovu na kufanikiwa kufanya nao kolabo japo nyimbo hizo hazikufanya vizuri.

Inasemekana Mr. Blue ndiye aliyempeleka Diamond Clouds Fm kutambulisha wimbo wa NENDA KAMWAMBIE na ndipo hapo Ruge akamsikia kwa mara ya kwanza na kuvutiwa na kipaji cha staa huyo na kuamua kumshika mkono, Kamwambie ikalia kwa ukubwa nchini hadi kuwa HIT.
_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad