Rayvanny Atangaza Kujitosa Kwenye Siasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Msanii huyo alipakia klipu kwenye ukurasa wake wa Tiktok alipoonekana amepiga suti kali nyeusi huku akisindikizwa kwenda kwa gari lake na walinzi, kuchora taswira kama ile ambayo huonekana kwa waheshimiwa.


Palisikika mtu mmoja akimfanyia utani kwa kumuita mbunge wa Mbeya Mjini, jambo lililootesha tabasamu usoni mwa msanii huyo ambaye aliamua kupasua mbarika kuwa siku za usoni atatathmini kujibwaga katika siasa katika kile alisema kuwa ni kuwafanyia wananchi kazi.


“Mwaka elfu mbii na ishirini na ngapi unagombea ubunge wa Mbeya Mjini?” alisikika akimuuliza mtu mmoja.


“Eeh Mungu akijaalia muda wowote tu nitawania ili kuwafanyia wananchi kazi ili tuhudumie taifa,” Rayvanny alijibu kwa mbwembwe zote kama mwanasiasa stadi.


Iwapo atafanikisha tamko hilo lake, Rayvanny atakuwa anajiunga na orodha ndefu ya wasanii wa Bongo ambao waliwahi jaribu karata yao katika siasa.


Alianza mwanamuziki mkongwe Professor Jay kujiunga siasa ambapo aligombea na kushinda ubunge wa Mikumi na kisha katika uchaguzi uliopita Mwana FA aligombea ubungwe wa Muheza na kuibuka mshindi.


Jokate Mwegelo pia aliteuliwa kama DC na hayati rais Magufuli, wadhifa ambao ameushikilia mpaka hivi sasa.


Msanii Harmonize pia aliwahi dokeza nia ya kuwania ubunge wa kwao Mtwara haswa baada ya kupata ushawishi na msukumo mkubwa kutoka kwa Magufuli lakini ndoto yake kama vile ilididimizwa kufuatia kifo cha rais huyo na tangu hapo Harmonize hajasikika sana akizungumzia kuhusu siasa.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad