AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi la polisi mkoani Kagera limefanikiwa kumkamata kijana Paschal Kaigwa (22) mzaliwa wa Kishogo Bukoba Vijijini, ambaye anatuhumiwa kumbaka na kumuua mke wa mwenyekiti wa mtaa wa National Housing kata ya Rwamishenye katika manispaa ya Bukoba, aitwaye Khadija Ismail (29)
Kamanda wa polisi mkoani Kagera William Mwampaghale amesema kuwa mtuhumiwa huyo alijificha katika vichaka na kwamba baada ya kukaa huko bila chakula, aliamua kutoka mafichoni na kwenda nyumbani kwa shangazi yake katika mtaa wa Katatorwansi ulioko katika manispaa ya Bukoba
Imeelezwa kuwa alipofika alikuta watoto ambao baada ya kumuona walipiga kelele na kuwezesha wananchi kumkamata.
"Njaa ilimtoa mafichoni akaenda kwa shangazi yake, lakini watoto aliowakuta pale walikuwa tayari wana taarifa, kutokana na taarifa zenu mlizozitangaza kuwa anatafutwa, tumemkamata juzi tarehe 19/02/2023 saa kumi jioni, tunaye tunamhoji na tutamfikisha kwenye vyombo vya kishera" amesema Kamanda Mwampaghale
Februari 13 mwaka huu majira ya jioni, kijana huyo ambaye alikuwa amepewa hifadhi nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa huo kutokana na kutokuwa na mahali pa kuishi, anadaiwa kumbaka na kumuua mke wa mwenyekiti na kisha kutoweka
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK