Breaking: Kiwanda Cha Jambo Plastic Kinawaka Moto Vingunguti

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Moto mkubwa umezuka mchana huu katika Kiwanda cha kuzalisha plastiki kiitwacho Jambo 11 kilichopo eneo la Vingunguti Jijini Dar es salam na hadi sasa unaendelea kuwaka kiwandani hapo.

Juhudi za kuuzima moto huo ambao bado chanzo chake hakijajulikana zinaendelea

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limesema hakuna madhara kwa Binadamu yaliyotokea kutokana na moto uliozuka Kiwanda cha kuzalisha plastiki cha Jambo 11 kilichopo Vingunguti Jijini Dar es salam lakini mashine na malighafi zimeungua na hadi sasa magari ya Zimamoto tisa yapo eneo la tukio kuendeleza mapambano ya kuuzima moto huo.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Ilala, Elisha Mugisha amenukuliwa akisema “Malighafi inayotumika kutengeneza plastiki na mashine zinazozalisha ndizo zinazoungua, tulichofanya ni kuzuia mashine ambazo hazijaathirika zisiungue na tumedhibiti moto usiende ghala jingine"

"Hapa tuna magari ya kuzimia moto tisa tunapokezana maji yakiisha wengine wanafuata Airport, tunapambana na kuzima moto kwanza, tukimaliza tutaanza uchunguzi kujua chanzo cha moto huu ni nini, kuna mashine kama saba zimeungua, hakuna Mtu aliyeumia au kupoteza maisha"
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad